REV. DR. ELIONA KIMARO: NIDHAMU NI HATIMA/ NGUVU YA KIUME
KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH
IBADA YA MORNING GLORY: THE SCHOOL OF HEALING
'HII NI KWARESMA:SIKU YA 12
27/ 02/ 2024
MADA:
NIDHAMU NI HATIMA
DISCIPLINE IS DESTINY
SOMO LA LEO: NGUVU YA KIUME
(GENDER DISCIPLINE)
Mwanzo 27 : 1 - 40
NENO KUU:
"Zitafakarini njia zenu"
(Consider your ways)
Hagai 1:7
Mwanzo 27 : 1 - 40
1 Ikawa Isaka alipokuwa mzee, na macho yake yamepofuka asione, akamwita Esau, mwanawe mkubwa, akamwambia, Mwanangu. Naye akamwitikia, Mimi hapa.
2 Akasema, Tazama, sasa mimi nimekuwa mzee, wala sijui siku ya kufa kwangu.
3 Basi, nakuomba, chukua mata yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo;
4 ukanifanyie chakula kitamu namna ile niipendayo, ukaniletee, ili nile; na roho yangu ikubariki, kabla sijafa.
5 Na Rebeka akasikia, Isaka aliposema na Esau mwanawe. Basi Esau akaenda nyikani awinde mawindo, ayalete.
6 Rebeka akamwambia Yakobo mwanawe, akisema, Angalia, nimemsikia baba yako akisema na Esau, ndugu yako, akinena,
7 Niletee mawindo, ukanifanyie chakula kitamu ili nile, na kukubariki mbele za Bwana kabla ya kufa kwangu.
8 Basi, mwanangu, sikiliza sauti yangu kama nitakavyokuagiza.
9 Enenda sasa kundini ukanitwalie wana-mbuzi wawili walio wema, nami nitawafanya chakula kitamu kwa baba yako, namna ile aipendayo.
10 Kisha utampelekea baba yako, apate kula, ili akubariki kabla ya kufa kwake.
11 Yakobo akamwambia Rebeka mamaye, Esau ndugu yangu ni mtu mwenye malaika, na mimi ni mtu laini.
12 Labda baba yangu atanipapasa, nami nitakuwa machoni pake kama mdanganyifu; nami nitaleta juu yangu laana wala si mbaraka.
13 Mamaye akamwambia, Laana yako na iwe juu yangu, mwanangu, usikie sauti yangu tu, enenda ukaniletee wana-mbuzi.
14 Akaenda, akawatwaa, akamletea mamaye. Mamaye akafanya chakula kitamu namna ile aliyopenda babaye.
15 Kisha Rebeka akatwaa mavazi mazuri ya Esau mwanawe mkubwa, aliyokuwa nayo nyumbani, akamvika Yakobo mwanawe mdogo.
16 Na ngozi za wana-mbuzi akamvika mikononi, na katika ulaini wa shingo yake.
17 Naye akampa Yakobo mwanawe mikononi mwake hicho chakula kitamu, na mkate alioufanya.
18 Akaja kwa baba yake, akasema, Babangu. Akasema, Mimi hapa, U nani wewe, mwanangu?
19 Yakobo akamwambia babaye, Mimi ni Esau, mzaliwa wako wa kwanza, nimefanya kama ulivyoniambia. Ondoka, tafadhali, ukae kitako, ule mawindo yangu, ili roho yako inibariki.
20 Isaka akamwuliza mwanawe, Imekuwaje umepata upesi namna hii, mwanangu? Akasema, Kwa sababu Bwana, Mungu wako, amenifanikisha.
21 Isaka akamwambia Yakobo, Karibu, tafadhali, ili nikupapase, mwanangu, nione kwamba wewe ndiwe mwanangu Esau, ama siyo.
22 Basi Yakobo akamkaribia Isaka, babaye, naye akampapasa, akasema, Sauti ni sauti ya Yakobo, lakini mikono ni mikono ya Esau.
23 Wala hakumtambua, kwa maana mikono yake ilikuwa kama mikono ya Esau, ndugu yake, yenye malaika; basi akambariki.
24 Akamwuliza, Wewe ndiwe kweli mwanangu Esau? Akasema, Ndimi.
25 Akasema, Niletee karibu nami nipate kula mawindo ya mwanangu, ili roho yangu ikubariki. Akamsogezea karibu, naye akala; kisha akamletea mvinyo, akanywa.
26 Isaka, baba yake, akamwambia, Njoo karibu sasa, ukanibusu, mwanangu.
27 Akakaribia akambusu. Naye akasikia harufu ya mavazi yake, akambariki akasema, Tazama, harufu ya mwanangu Ni kama harufu ya shamba alilolibariki Bwana.
28 Mungu na akupe ya umande wa mbingu, Na ya manono ya nchi, Na wingi wa nafaka na mvinyo.
29 Mataifa na wakutumikie Na makabila wakusujudie, Uwe bwana wa ndugu zako, Na wana wa mama yako na wakusujudie. Atakayekulaani alaaniwe, Na atakayekubariki abarikiwe.
30 Ikawa Isaka alipokwisha kumbariki Yakobo, na alipokuwa Yakobo ndiyo kwanza ametoka mbele ya Isaka, baba yake, mara Esau ndugu yake akaja kutoka katika kuwinda kwake.
31 Naye pia amefanya chakula kitamu akamletea babaye, akamwambia baba yake. Babangu na aondoke, ale mawindo ya mwanawe, ili roho yako inibariki.
32 Isaka, baba yake, akamwuliza, U nani wewe? Akasema, Mimi ni mwanao, Esau, mzaliwa wako wa kwanza.
33 Isaka akatetemeka tetemeko kuu sana, akasema, Ni nani basi yule aliyetwaa mawindo akaniletea? Nami nimekwisha kula kabla hujaja wewe, nikambariki; naam, naye atabarikiwa.
34 Esau aliposikia maneno ya babaye, akalia kilio kikubwa cha uchungu sana, akamwambia babaye, Nibariki na mimi, mimi nami, Ee babangu.
Mhubiri: Rev. Dr. Eliona Kimaro
Kwa maombi na ushauri :
Mch. Kiongozi: Dr. Eliona Kimaro
Simu: +255 655 516 053, +255 754 516 053
Пікірлер: 21
Kama nyumba za ibada zingetufundisha wanaume na WANAWAKE nguvu zetu tungeishi kwa furaha na upendo kila mtu angekaa kwenye njia yake shetani asingekuw na nguvu kwa baazi ya watu❤❤❤
Huyu mtumishi anaitaji kujengewa mnara,akumbukwe vizazi na vizazi,baba ndiye mtoa baraka sio mamaaaaa🤲🤲🤲🙏
@leonardnyange7152
5 ай бұрын
Uo ndo UKWELI 🎉
My eyes began to see more when I started following your sermon Baba, God bless you
Baba mchungaji unanena ukweli. Mungu akupe hekima ya kutukuza na neno la Mungu. Im blessed to follow & listen to you from +254
Amina mtumishi
Mungu akubariki San mtumishi.
Eye opening, bless you Reverend.
Asante mtumishi wa mungu
Nimeyapitia yote hayo yasikukute aise nilikua nakiu yakumuona baba yangu finaly i met him GLORY TO GOD,
Be blessed Pastor
Amen
🇮🇱Mchungaji "umepiga" Hakika kakika unayoyahubiri yapo. Mungu akubariki sana Mchungaji Kimaro.
Asante Kwa neno
Mataifa wamsujudie Bwana.
Ameen
Ameeeen Baba, Mungu akupe Maua yako mengiii
Hallelujah hii nimewahi kuhubuli agenda hii aliye beba baraka ni mwanaume nilipigwa madongo sana nimefurahi sana kuona mtu mkuu kama huyu anazungumuzia mle mle Dunia sikia hii
@miriamdavis3893
5 ай бұрын
Uelewa ,ukiona unapigwa nyamaza
Esau alipoongoka alivunja kongwa la ndugu yake.
Amen