Meena Ally Afunguka Yote, Kujiunga Clouds, Familia Na Maisha Yake | SALAMA NA MEENA PART 1

Ойын-сауық

#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
MARASHI YA KARAFUU…
Jina lake halisi ni Muhaymeena Ally na kwa kifupi aliona Meena litamfaa sana na si Amina kama watu wengi wanavyodhani. Mzaliwa halisi wa Zanzibar na ni mtoto wa Stone Town kabisa. Kutoka alikozaliwa Meena na nilipozaliwa mimi si mbali kabisa, kwao Malindi karibu kabisa na bandarini na mimi kwetu ni Kiponda, wakati Meena anazaliwa mwaka 1993 mimi nilikua darasa la sita, msichana kabisa na pengine nilishaanza kuandikiana barua na kichimvi na kina Murad 🤣.
Mimi na yeye tumefahamiana hapa Dar es Salaam lakini, sina hakika kama wazazi wetu wanajua maana bado sijamuuliza Mama yangu ila nna hakika wa asilimia 99 kwamba Kaka zangu (ambao wengi wao ni wavuvi) wanawajua wazazi wake na pengine shangazi na wajomba zake, mtaa ambao Meena kazaliwa ndo njia wanayopita kwenda Pwani so uhakika huo nnao kwa asilimia hizo. Lately mimi na yeye tumekua karibu, uzanzibari pengine unachangia kwa kiasi kidogo ila binafsi zaidi ni kwasababu na admiration ya kazi zetu kwa kila mmoja wetu. Wakati Meena anakuja EATV mimi sikumbuki vizuri na nadhani zilikua ndo siku zangu za mwisho mwisho kuwa muajiriwa pale au pengine nlikua tayari nlikua nafanya mambo yangu pembeni kwa kupitia Mkasi TV.
Nilifurahia kila sekunde ya maongezi yetu haya kwasababu nilikua naongea na Rafiki yangu na ki ukweli ilikua inatakiwa yafanyike siku nyingi tu ila kama unavyojua, sisi binadamu tunapanga mambo yetu ila Mwenyezi Mungu ndo hutupa nguvu na wasaa wa kutufanya tuyatekeleze kwahiyo wakati huu ndo ulikua wakati sahihi.
Kama mwezi umepita Meena alipata mitihani kwenye mitandao ya kijamii baada iliyokua inalazimishwa iwe video yake akiwa anafanya ngono kutambaa mitandaoni. Kama Dada ilinishtua mara ya kwanza na uzuri ni yeye mwenyewe ndo alinitumia, ukimuangalia yule Dada kwa pembeni unaweza kudhani ni yeye ingawa kama unamfahamu Meena kwa ukaribu basi utajua kabisa yule si yeye. Mtihani ulikua mkubwa, mtihani wa kuwaelezea binadamu ambao baadhi yao walikua wanataka yule awe yeye nao walikuwepo lakini walikua hawataki kuamini nao pia tulikua wengi tu. Mawe mengi yalirushwa na ilihitaji Meena awe kwenye ubora wake, kuto panic na kufanya yote yaliyokua yanatakiwa kufuatwa ki SHERIA na mengine tuiachie Mamlaka inayohusika ambao naamini bado wanaendelea na kumtafuta aliyeanzisha uvumi ule na yangu imani watampata ili awe mfano kwa wengine.
Sina hakika sana na nasema hivi kwasababu kwa mtu mwenye imani na akili timamu hawezi kufanya unyama kama huu kwa mtu mwengine ambae hana ubaya nae. Madhara yanayokuja na shutuma kama hizi ni makubwa sana, ki akili na ki utu na ki biashara. Athari zake zinaweza kuwa za muda mrefu kuliko wengi wanavyo dhania.
Humu nilimuelewa vizuri, utulivu wake kwenye kujibu maswali na jinsi alivyokua amejibeba, mmoja anaweza kuangalia kwa kujifunza kutoka kwake, Meena ana kila kitu ambacho kinaweza kikamfanya yeye aweze kutimiza ndoto zake, kuwa chochote kile ambacho atapewa au atapata nafasi ya kukifanya, kuanzia kwenye filamu mpaka yote yale ambayo anatamani kuyafanya na anaweza kuyafanya kwa asilimia 100, ambayo sina shaka atayapa na pengine zaidi.
Humu tunamzungumzia Marehemu Bibi yake ambaye kifo chake kilimuathiri kwa kiasi kikubwa na jinsi ambavyo alijikwamua kutoka kwenye wimbi hilo la msongo. Maelewano yake na wazazi wake ni kitu cha kumfanya mtu ajifunze kutoka kwake, najua si kila mmoja wetu ana mahusiano ya aina hii na wazazi wake ila kwa kuskiliza naamini utapata ujumbe flani. Heshima na kujituma kwake anapokua anafanya kazi pia itaiskia humu, kujitoa kwake na jinsi anavyoangalia na kujifunza mengi kwa kuwasoma watu na nafasi zao kunamfanya aweze kufika mbali, na yangu matumaini nnayoyaona mimi kwake basi na yeye anayaona hivyo na zaidi. Kazi yetu sisi ni ku enjoy tu kwa kuangalia safari yake ya kikazi na kushuhudia mafanikio yake tele yajayo In Shaa Allah.
Enjoy hii session kama ambavyo umekua uki enjoy na kujifunza mengi kutoka kwa wengi waliopita na wengi wajao. Mungu katubariki na watu wengi wa aina hii ambao wako mbele yetu, maisha yao ni darasa tosha kwetu sote. Ni vyema yale tutakayo yapenda tukayaweka na sisi katika maisha yetu ili tufike mbali zaidi.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
‪KZread Link bit.ly/KZreadSalamaNa
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz

Пікірлер: 98

  • @saidmohamed4619
    @saidmohamed46192 жыл бұрын

    Aisee leo nimeenjoy sana...two kids from Zanzibar in one place...hapo ni matani ya kikwetu tu...

  • @bongotvonline4883
    @bongotvonline48832 жыл бұрын

    Unajua SALAMA wewe ni shida sana, sina la kusema kuhus wewe. Ila kwa wanaoelewa wanajua kazi ilivyo kumhoji MTANGAZAJI MWENZIO. All the best Salama.

  • @Kevin_davi
    @Kevin_davi2 жыл бұрын

    Salama naomba hichi kipindi cha salama na kirudi kwenye channel ya East Africa television kama ilivyokuwa hapo awali sisi wanyonge hatuna pesa ya kununua dstv bei yao ikoo juu sana

  • @Wachuoni
    @Wachuoni2 жыл бұрын

    I think this kind of Interview suits you better, naifananisha hii na Zuhura Yunus, imejaa upendo, utani, uhuru, ucheshi, hisia za ukweli kabisa kutoka moyoni. na kwa hii pekee nimependa sana vionjo vya lugha za Mina ... kama "Dada Judi acheke", .... it was great 👍.... keep it up !

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum72792 жыл бұрын

    Salama ''tuna omba Mlete bikilala! na mzee kikalala 😘na muwandishiw wao' wa kombolela 🔥🔥

  • @drwebangila
    @drwebangila2 жыл бұрын

    Navutiwa sana Meena. Looks smart and intelligent. Kila la kheri Salama na Meena. Naamini Mkiungana Nchi itasimama.

  • @maryshirima1234
    @maryshirima12342 жыл бұрын

    I love the way Meena answers the questions... 👌💚

  • @odrianinicolaus5353
    @odrianinicolaus53532 жыл бұрын

    Tuletee, Yule Mbunge Kishimba wa Bungeni au Mhe.Msukuma Salama

  • @badalichauchau6983
    @badalichauchau69832 жыл бұрын

    Nampenda sana huyu dada kwasababu hajawahi kuzungumza maneno ya ovyo

  • @iammichaellukindo
    @iammichaellukindo2 жыл бұрын

    Nimefanya kazi na meena EATV na Clouds lakini baada ya kumsikiliza hapa nahisi kama sasa ndio nimemjua angalao. And hongera Meena. I know what happened to you EATV. Mungu amekupa nafasi keep Going

  • @mongai001
    @mongai0012 жыл бұрын

    To be honest this young lady she always make me laugh peace and love

  • @stevennyondo2215
    @stevennyondo2215 Жыл бұрын

    Kwenye lafudhi nakubali huyu dada. First time namuona nlijua chuga girl.

  • @antonymwaniki6248
    @antonymwaniki6248 Жыл бұрын

    I really like Meena's voice.

  • @mkaapwekekariakoo6417
    @mkaapwekekariakoo64172 жыл бұрын

    asante sana Salama.... natamani siku moja uingie mtaani utuletee mtu ambaye si maarufu lakini, ambaye ataweza kufanya usaili nawe. hata kama si kumfanya maarufu lakini itakuwa pia namna ya kuhamasisha watu kuwa kile wanaamini. Kazi nzuri sana, ni lini utajihoji hahahaaa

  • @bish_daddiyao
    @bish_daddiyao2 жыл бұрын

    Nice interview.. Bring Zuchu I have been Searching for Long🙌🏾🇰🇪💕

  • @rodrickmataba8999
    @rodrickmataba89992 жыл бұрын

    Habari, Hujambo...😀😀😀 leo hii salamu hatujaipata

  • @maryshirima1234
    @maryshirima12342 жыл бұрын

    Ace jay keep up the good work...👌💚

  • @mohamednaaman188
    @mohamednaaman1882 жыл бұрын

    Masha Allah interview nzuri #Zanzibar 🔥

  • @victormwakipesile6990
    @victormwakipesile69902 жыл бұрын

    Tunaomba ya Dina marious

  • @chiticollemans
    @chiticollemans2 жыл бұрын

    Please bring Ghalib (GSM) and Flaviana Matata

  • @user-gi1ez6fc1y
    @user-gi1ez6fc1y2 жыл бұрын

    Can't wait salama na Millady

  • @lastsimbatv1497
    @lastsimbatv14972 жыл бұрын

    U kill it salama i love u mwaaaah beautiful

  • @bobanthony1326
    @bobanthony13262 жыл бұрын

    Quite funny; had a good laugh.

  • @didahbebe3866
    @didahbebe38662 жыл бұрын

    I really like the answers za meena and she's so smart ma sha allah

  • @neemapetro8188
    @neemapetro81882 жыл бұрын

    I love mena jmn uwii❤️❤️❤️❤️

  • @alphonsinedusabe3590
    @alphonsinedusabe35902 жыл бұрын

    🤣🤣🤣 jmni meena wew 💥😍

  • @yetromtambulo3452
    @yetromtambulo3452 Жыл бұрын

    Keep it up

  • @saumusalimuhassan2499
    @saumusalimuhassan24992 жыл бұрын

    Nakukubali sana Meena

  • @chardoAmos4476
    @chardoAmos44762 жыл бұрын

    Mimi naomba ufanye interview na milard ayo please

  • @zhaujiakashindi6617
    @zhaujiakashindi66172 жыл бұрын

    Nawapenda sana…❤️❤️

  • @el-chicosfootballdevelopme7411
    @el-chicosfootballdevelopme74112 жыл бұрын

    Iyo lafudh anayoigiza ni ya joti si ya kizanzibari. Wazanzibari hawaongei hvo.

  • @princessbim6096
    @princessbim60962 жыл бұрын

    Salama naa zuchu ndo umeificha shoga yngu

  • @janethsuleiman2445
    @janethsuleiman24452 жыл бұрын

    Nimecheka sana

  • @davidnchoji
    @davidnchoji2 жыл бұрын

    I love you Da Salama, am here just for you and that beautiful Lady Meena❤️🙌🏽

  • @alphredinaalphonce7043
    @alphredinaalphonce70432 жыл бұрын

    💕🥰

  • @mohamedhamad2374
    @mohamedhamad23747 ай бұрын

    Sister salama mambo nimefatilia mahojiano unayofa nya naona unafanya na watu ambao ni maarufu vipi wasio kuwa maaarufu

  • @shahabdul1126
    @shahabdul11262 жыл бұрын

    when will you upload Salama na Zuchu? we need it here

  • @mtanzaniahalisimungunimwem673
    @mtanzaniahalisimungunimwem6732 жыл бұрын

    Nawapenda sana wote jamani

  • @ishakafaki3501
    @ishakafaki35012 жыл бұрын

    Rangi nyekundu Kwa asie onaa nikumwambia afinge macho then awashe tochi machoni mwake then utamwambia hiyoo ndio rangi nyekundu

  • @santruninichamy4974

    @santruninichamy4974

    2 жыл бұрын

    Umetishaaa... We kichwa

  • @dilipdab3714
    @dilipdab37142 жыл бұрын

    Kweli.leo.munachoweyaa

  • @mariagodfrey2028
    @mariagodfrey20282 жыл бұрын

    😀😀😀😀😀

  • @rosegideon336
    @rosegideon336 Жыл бұрын

    Mfike Mbali.

  • @ayeeshasuleiman8826
    @ayeeshasuleiman88262 жыл бұрын

    Hahaaa nimefurah

  • @loysirikwa5052
    @loysirikwa50522 жыл бұрын

    Upload Salama na Adam Mchomvu

  • @fahadfahmy
    @fahadfahmy2 жыл бұрын

    Wazenji united.

  • @tofikijafary8470
    @tofikijafary8470 Жыл бұрын

    Mmm

  • @bjzee1981
    @bjzee19812 жыл бұрын

    Karo za chooni sio round but ni oval

  • @bjzee1981
    @bjzee19812 жыл бұрын

    Kumbe tuko wengi. Na ndio kilicho nifanya nijue lugha nyingi.

  • @shedyali964
    @shedyali9642 жыл бұрын

    Samahan salama darajan hamuna round kuna nondo na harufu mbaya

  • @dilipdab3714
    @dilipdab37142 жыл бұрын

    Ww.meena. salam.leo.munanichekesha.kweli

  • @alantonio855
    @alantonio8552 жыл бұрын

    Mwijaku next time

  • @fortunathabarabara8471
    @fortunathabarabara84712 жыл бұрын

    salama na wema sepetu

  • @sabraridhwan2858
    @sabraridhwan28582 жыл бұрын

    Salama badilisha nguo hizo kila Siku nyeusi kama upo msibani

  • @salumbabu

    @salumbabu

    2 жыл бұрын

    Acha makasiriko,,, 😁😁😁😁

  • @meky9404
    @meky94042 жыл бұрын

    tunamwomba na msuvaaaa

  • @tamrikznz7583
    @tamrikznz75832 жыл бұрын

    Nyinyi Wapemba Mnaitwa Huku Kwenu.

  • @dilipdab3714
    @dilipdab37142 жыл бұрын

    Sie.hivyo.vilikuwa.ndio.yeyetu.vifundo.vya.miwaa.salama.na.meena.lakini.sahivi.kifundo.kinalipwaa

  • @ycb_yakoub3584
    @ycb_yakoub35842 жыл бұрын

    Swala la kurithi lafuzi hii ni kawaida kwa wamwambaoo asilimia 75% wapo hivo

  • @kharounngavason8012
    @kharounngavason80122 жыл бұрын

    Kwa MEENA tena ufika hapo

  • @abdullahhamed2197
    @abdullahhamed21972 жыл бұрын

    Tunaomba ya salah wa GSM

  • @fatumahilaly9911
    @fatumahilaly99112 жыл бұрын

    SALAMA KIPENZI MBONA YA ZUCHU HUJAIPOSTI JAMANI IPOSTI BASI JAMANI🥺

  • @keifatuke99

    @keifatuke99

    2 жыл бұрын

    Nimeosubiri ya Zuchu mpaka nimechoka

  • @hamedabashir9
    @hamedabashir92 жыл бұрын

    Tunaomba ya zuchu

  • @oscarmwakibinga1142
    @oscarmwakibinga11422 жыл бұрын

    Aliezaliwa haoni kwani anajua rangi ya damu?

  • @user-eo7ug2tg9r
    @user-eo7ug2tg9r2 жыл бұрын

    My love meenaally😍😍😍😍

  • @talazain1017
    @talazain10172 жыл бұрын

    Binafsi

  • @lareineminah1353
    @lareineminah13532 жыл бұрын

    Salama na zuchu lini?

  • @dilipdab3714
    @dilipdab37142 жыл бұрын

    Salama.lakini.hapo.zamani.kama.hujaokotoa.vifundo.forodhani.bc.hakuzaliwa.zeji.itakuwa

  • @razackkalanje5049
    @razackkalanje50492 жыл бұрын

    wekeni ya zuchu

  • @razackkalanje5049
    @razackkalanje50492 жыл бұрын

    Tuwekeeni ya zuchu

  • @mwanaidikhatibu4726
    @mwanaidikhatibu47262 жыл бұрын

    Tunamumba dinaa marios

  • @dilipdab3714
    @dilipdab37142 жыл бұрын

    Wanaokota.vifundo.sio.miwaa

  • @oyay2821
    @oyay28212 жыл бұрын

    Haya maneno ya kuzungu kama inferior, insight au relate waTz wanafahamu?

  • @kdloon2030

    @kdloon2030

    2 жыл бұрын

    Tueleze wewe mzungu

  • @jean-Robert
    @jean-Robert2 жыл бұрын

    Tunaitaji interview yako na zuchu aipo youtube kwanini?

  • @dilipdab3714
    @dilipdab37142 жыл бұрын

    Kifundo.chamuwaa

  • @saidahmed9688
    @saidahmed9688 Жыл бұрын

    meena tunakupenda

  • @barikilangoy4737
    @barikilangoy47372 жыл бұрын

    Utuletee na diwani wa mama ashura

  • @jrsaid4270

    @jrsaid4270

    Жыл бұрын

    We kijana acha masihara 🤣🤣

  • @barikilangoy4737

    @barikilangoy4737

    Жыл бұрын

    @@jrsaid4270 sio masihara naona kama zinaendana tufanye kama hii episode 1 afu ya diwani wa ashura episode 2

  • @jrsaid4270

    @jrsaid4270

    Жыл бұрын

    @@barikilangoy4737 🤣🤣🤣🤣 Mr Pimbi he!? 🤣🤣

  • @ashurantandu1799
    @ashurantandu17992 жыл бұрын

    Kuongea kingereza ndo kupotezana mada

  • @tuesdaymeli8458
    @tuesdaymeli84582 жыл бұрын

    😄😄😄😄😄😄😄😄 hawa wote mm nawapenda

  • @fahadfahmy
    @fahadfahmy2 жыл бұрын

    Kiswahili fasaha

  • @Boaz22
    @Boaz222 жыл бұрын

    Alisikiaje baada yakuhusishwa kwenye video ya Ngono???😩

  • @maryshirima1234

    @maryshirima1234

    2 жыл бұрын

    Part 2 kajieleza.

  • @josephmuchiri3180
    @josephmuchiri31802 жыл бұрын

    Mbona sasa anachekacheka

  • @faizadiriye1384
    @faizadiriye13842 жыл бұрын

    Salama mbona humuweka zuchu

  • @mwanajumamohammed6327
    @mwanajumamohammed63272 жыл бұрын

    Meena ni mtoto wa master j ama mm ndio sijui

  • @fathimaf1048

    @fathimaf1048

    2 жыл бұрын

    Hapana dear meena ni mtu wa Zanzibar na Master j ni mtu wa kilimanjaro wapo kikazi

  • @mwanajumamohammed6327

    @mwanajumamohammed6327

    2 жыл бұрын

    Asante dear...sikuona ubaya kuuliza...maana sijui na misio Mtanzania...ni mkenya na pia cko Kenya niko safar

  • @mtanzaniahalisimungunimwem673

    @mtanzaniahalisimungunimwem673

    2 жыл бұрын

    @@mwanajumamohammed6327 mhhhh

  • @bjzee1981
    @bjzee19812 жыл бұрын

    Hiyo hata sio kichekesho. Bora mgombea urais wa Kenya wajakoya

  • @kingkinye1419
    @kingkinye14192 жыл бұрын

    Singeli hii Kali sanakzread.info/dash/bejne/gKmtq9lpj67XctY.html

  • @christopherpeter3112

    @christopherpeter3112

    2 жыл бұрын

    Zuchu lini

Келесі