KWANINI HAVITOKEI KWA WAKATI (I) - PASTOR SUNBELLA KYANDO

Mathayo 25:1-12
Kuna aina mbili za wanawali katika hii mistari.
(a)Wanawali wapumbavu
(a)Wanawali werevu
Wanawali wapumbavu ni wale ambao hawakubeba mafuta ya ziada,na wale werevu ni ambao waliobeba mafuta ya ziada.
Wanawali wapumbavu hawakubeba mafuta ya ziada kwa sababu walipiga hesabu ya muda ambao bwana arusi atafika na muda harusi itatumia yale mafuta waliyobeba yangewatosha.Kwahiyo hawa wanawali hawakuwa na kosa.
Wanawali werevu hata kama walijua muda ambao bwana arusi atakuja na harusi itatumia,walijiandaa kwa lolote na ndio maana wakabeba mafuta ya ziada.
Kitu cha kwanza kutokea ni bwana arusi kukawia,hii inamaanisha kuna kitu kilitokea kikamchelewesha kufika.Na ukimuuliza atakupa sababu ya kimwili kabisa.Bwana arusi anaingia kwenye matatizo kwa sababu kuna watu ambao amewaalika ambao shetani hataki wafanikiwe.Kuna vita ambazo tunapigana sio kwa sababu shetani ana shida na sisi bali watu ambao tumewaingiza kwenye maisha yetu.Unapigwa wewe kwa sababu msaada ambao unataka kuwapelekea shetani hataki msaada uwafikie.
Kitu cha pili wanawali wakalala usingizi.Neno linasema wakasinzia wote.
Ukisinzia unaanza kutokufahamu kile kinachoendelea katika eneo ambalo una changamoto(unazubaishwa).Unaweza kujua kabisa hilo eneo una shida lakini hufanyi chochote kutoka kwenye hiyo shida.
Ukishatoka kwenye kusinzia unafuata hatua ya kulala.Ukifikia hatua hii unaweza kuwa kanisani na somo linalofundishwa linakuhusu kabisa,lakini kila ukisikiliza unamuona mtu mwingine unayemjua kuwa hilo somo linamhusu na hujioni wewe.
Ukifika hatua hii jua umelala kabisa.
UNAWEZA WASILIANA NASI AU KUTUMA SADAKA YAKO KWA NAMBA HII : 0657 173 322
Unaweza kutufuatilia katika mitandao yetu ya kijamii
Like our Facebook: / therealityof. .
Follow our Instagram: / realityofch. .
Subscribe our KZread: kzread.info/dron/67L.html...
Also Subscribe Roc worshippers youtube channel: / @rocworshipperz

Пікірлер: 26

  • @loyceyahya2622
    @loyceyahya26229 ай бұрын

    Amen Amen nazidi kufunguliwa Kwa hizi jumbe zako Mtumishi wa MUNGU uishi maisha marefu uzidi kutufungua zaidi

  • @FadhiliMaganga
    @FadhiliMagangaАй бұрын

    Ubarikiwe baba Mungu akutunze sanaa❤

  • @catherinemwakibinga2285
    @catherinemwakibinga22852 жыл бұрын

    Nakupenda sana baba yangu..🙏🙏🙏 Mafundisho yako yana nijenga.. Ubarikiwe zaidi na Mungu..

  • @malaikalihuda2831
    @malaikalihuda2831 Жыл бұрын

    Amina amina mtumishi

  • @petermunuo1657
    @petermunuo1657 Жыл бұрын

    Amen mtumishi barikiwa sana

  • @LuluJuma-mt2dh
    @LuluJuma-mt2dhАй бұрын

    Thank

  • @user-qo8tm4sn3s
    @user-qo8tm4sn3s9 ай бұрын

    Asante kwa ufahamu huu

  • @mwlwilibaththomas6936
    @mwlwilibaththomas69362 жыл бұрын

    Mungu akubariki sana baba, umekuwa daraja kubwa kwangu kupitia masomo yako ninayofuatilia na hili somo limeniongeza sana.

  • @josephatjoseph1755
    @josephatjoseph17552 жыл бұрын

    Asante sana kwa masomo mazuri ila naomba unieleweshe huu mstari unachanganya wengi. Amina KUMBUKUMBU LA TORATI 22:5 Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanamume, wala mwanamume asivae mavazi ya mwanamke; kwa maana kila afanyaye mambo hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako.

  • @giftmollel7788
    @giftmollel77882 жыл бұрын

    Kwakelii ni tusubirii kwa Yesu

  • @suleimandaugd892
    @suleimandaugd8922 жыл бұрын

    Upo vizuri mtumishi wa mungu ubarikiwe sana na beans yesu

  • @monicahmwalozi
    @monicahmwalozi Жыл бұрын

    Amen 🙏 mtumishi kwa hili somo umenifungua macho yangu ya kiroho 🙇‍♀️

  • @claranewaho1251
    @claranewaho12512 жыл бұрын

    Nakuelewaga Mimi had basi

  • @jojoba2633
    @jojoba26332 жыл бұрын

    This series has been a blessing to me to understand the massage 'coz it's been horrible histories of my life thank God for I've got the answer thank you for sharing

  • @aminaalid9745
    @aminaalid9745 Жыл бұрын

    Nimependa sana hili somo

  • @monicahmwalozi
    @monicahmwalozi Жыл бұрын

    Mungu atusaidie

  • @josephmuhindo7393
    @josephmuhindo7393 Жыл бұрын

    Amen ameeeen🙏🏼🙏🏼🙏🏼🙏🏼🙏🏼🙏🏼

  • @eliyalucas2188
    @eliyalucas21882 жыл бұрын

    Be blessed Pastor, what a powerful revelation.

  • @carolinengondo2698

    @carolinengondo2698

    2 жыл бұрын

    Pastor nimebarikiwa.I reside in Kenya 🇰🇪. Pray for me,my marriage, and my workplace. I need a break through.

  • @user-gt8ys2cl2u
    @user-gt8ys2cl2u Жыл бұрын

    You open my eyes man of God...be blessed

  • @danstonecool1734
    @danstonecool17342 жыл бұрын

    neno limenitia nguvu zaidi

  • @mariamsiwale9636

    @mariamsiwale9636

    2 жыл бұрын

    Asante kwa mafundisho mungu akubaliki

  • @elinemchome9067
    @elinemchome9067 Жыл бұрын

    Mafundusho mazuri yamenipa kuelewa maana ya mameno ya Mungu nimepata kitu.

  • @meclinanyamwihura3748
    @meclinanyamwihura37482 жыл бұрын

    Mh

  • @doreengaspar6772

    @doreengaspar6772

    Жыл бұрын

    Barikiwa sana mtumishi

  • @asifiwemjujulu8884
    @asifiwemjujulu88842 жыл бұрын

    Mungu atusaidie