Biden kuwaondoa mashaka viongozi wa Afrika kuhusu nia ya Marekani kwa bara hilo
Rais Joe Biden atakuwa mwenyeji wa dazeni ya viongozi wa Afrika hapa Washington wiki hii. Wakati ambapo White House itakuwa ikiangalia kupunguza pengo la uaminifu na Afrika -ambalo limekuwa kubwa baada ya miaka kadhaa ya mashaka kuhusu nia ya Marekani kwa bara hilo.
Mkutano huu utakuwa ni mkusanyiko mkubwa sana wa kimataifa hapa Washington tangu kuanza kwa janga la Covid-19. Maafisa wanawaonya wakazi kuheshimu vizuizi vya barabarani na kuimarishwa kwa ulinzi wakati wakuu na viongozi wa nchi 49 pamoja na Biden wakiwa wanazunguka mjini.
#VOAUSAfricaLeadersSummit
#USAfricaLeadersSummit, #USAfricaLeadersSummit22
- - - - -
#VOASwahili
Sauti ya Amerika - Idhaa ya Kiswahili inawafikia zaidi ya watu milioni 100 wanaotembelea tovuti, mitandao ya kijamii, radio na televisheni zetu. Tunawasilisha maudhui kuhusu Afrika Mashariki na Kati kwa nchi takriban 11 huko Afrika na wale walioko ughaibuni na kwingineko duniani. Vipindi vyetu vimejikita katika maudhui mbalimbali ikiwemo habari, vijana, wanawake, siasa, sayansi, teknolojia, afya, biashara, michezo, muziki na burudani na pia tunawashirikisha wasikilizaji wetu.
Пікірлер: 10
Anataka kuwatia mashaka ama kuwaongezea mashaka.. Coz yake yanaelekea kumshinda.. Zid ya urusi so anakuja huku kwetu ambako bado hatujaamka ili apate kuzid kutukandamiza.. Kwann wanakimbilia Africa.. Viongozi wetu wa Africa AMKENI.. URUSI KATUONYESHA NJIA.. TUSIWE TEGEMEZI
Hahahahaha, ilikwa ivo pia wakati wa ukoroni
Anataka kuwaongea tena mashaka mengi na mateso zaidi
Wa congo na WA Rwanda wasikilizane ili amani irejeye waace kuuwana Bure, vicace ama vingi wacangie.
Tushasema tupo na urusi hatuwataki ulaya na Americans
Mshachelewa,tayari china ishahozi, na hamuwezi, kuizidi china kiushawishi,
Sisi atuwatak mmesha tutesa San mtu ache
@mosesmwailenge5192
Жыл бұрын
Asante umeongea vizuri nimekupenda bulee MUNGU wambinguni akubaliki saana 🙏🙏🙏🙏💕
@mosesmwailenge5192
Жыл бұрын
Hakika hakika hatuwataki